Thursday, September 16, 2010

TUSIMA YAWAPIKU MAHARUSI KATIKA UKUMBI WA AGA KHAN

Bwana Harusi akiwa na vazi la joho
TUSIMA ilijibwaga katika ukumbi wa Aga Khan mjini Mambasa wakati wa Idd Ul Fitr na kuonesha mapambo ainati ya maharusi wa Kiswahili.

Maonesho haya yaliyoandaliwa na wachapishaji wa jarida la EVE yaliazimiya kuwaleta wapambaji pamoja na washonaji wa nguo na mapambo mengine ya maharusi kuonesha bidha hizo ili wapate kujulikana na kujenga uhusiano na wateja wapya. Maonesho haya yalifanyika kuanziya tarehe 10 hadi 12 Septemba 2010.

TUSIMA ilionesha mavazi ya bwana na bibi harusi wa Kiswahili yakiwamo majoho, magauni, vibeti, mikoba, marinda na bidhaa nyinginezo za maharusi. Wageni wengi walitembeleya maandalizi ya TUSIMA na kupendezewa nayo. Wawakilishi wa TUSIMA walijijulisha kwa wateja wengi wapya ambao walifurahiya bidhaa hizo. Wawakilishi hawa walitiwa moyo sana na maonesho haya hata wakahamasika kufanya yao au kushiriki tena katika maonesho kama haya mwakani.

Wednesday, September 15, 2010

MWITO WA IKHTISARI WAKOMA

Jumba la ofisi kuu ya RISSEA
Kadhiya ya mwito wa ikhtisari kwa kongamano la kimataifa la RISSEA litakalofanyika hapo Novemba mwaka huu umekoma. Jumla ya ikhtisari 25 zilipitishwa na Kamati ya Urejelezi na waliyofaulu tayari wameshajulishwa kutayarisha makala zao kamili. Mawanda yaliyogusiwa kuligana na ikhtisari hizo ni pamoja na ilimu insi, isimu, historiya, fasihi, dini na uchumi wa ardhi. Makala kamili yanatarajiwa mnamo tarehe 8 mwezi wa Novemba mwaka huu.

Thursday, September 2, 2010

ISTILAHI ZA KISWAHILI

ISTILAHI       KISAWE      UFAFANUZI

Global       Zingiro           Global kwa Kiswahili itawakilishwa na zingiro kwa sababu 
                                      ni kitu mviringo au duwara.

Scanner    Tambazo        Tambazo kuwakiliswa na scanner lina maana kutaza au 
                                     kueneza.

Internet     Ungamano      Ungamano lina maana internet kuunganiisha au 
                                      kuwaunganisha watu mbali mbali  kuweza kusikilizana.
                                    
Office    Ukurungwani     Ukurungwani lina maana ya office,mkurungwa ni officer 
                                    neno la zamani la Kiswahili

Radio      Mwengoya      Mwengoya lina maana ya radio kutokana na neno mwengo 
                                    kwa kiengereza ni echo utanda kazi wake ni sauti ya kuja 
                                    kutoka mbali uliko wewe maana mwengo wa 
                                    kuya = mwengoya.

Computer  Ngamizi    Computer linawakilishwa na neno ngamizi kwa ajili ya utenda 
                                kazi  wake maana nikupokeya ukitiacho cha meza ikiwa ni 
                                vitabu ni maandishi anajaza bila ya kukataa ile iharibike.

Mouse   Kitauzi        Mouse linawakilishwa na kitauzi maana kifaa chenya 
                                kuchagua unachotakakukiona kukivuta kije mbele yako 
                                katika ngamiza

Fax      Pepesi        Fax linawakilishwa neno la Kiswahili pepesi lina maana 
                              ya mfano wakupepesa utenda kazi wake.

E-mail   Baruwa pepe E-mail linawakilishwa na baruwa pepe yaani baruwa yenye
                                kupeperushwa kwa njia ya Kiamu pepe ni umeme.

Ray        Uka         Ray linawakilishwa na uka katika matumizi ya kumepambauka
                             kwa lahaja ya Kiamu, kwa kisanifu kumepambazuka kwa wingi
                             ni nyuka.

Picture  Uyoo          Picture linawakilishwa na uyoo kutokana na kuiyowa.


Science  Ulimbe       Science linawakilishwa na ulimbe lenya maana ya elimu
                               ya ulimwengu na viumbe.

Psychology Ushunuzi  Psychology linawakilishwa na ushunuzi lenya maana
                                  ya kushuwa yaliyomo ndani kudhihirika nje.


No: Prof. Ahmed Sheikh Nabahany
Swahili consultant
TUSIMA



Tuesday, August 31, 2010

SHEREHE YA KUSHUWA JARIDI LA KWANZA LA TUSIMA

Wageni mashuhuri waliohudhuri tamasha za ushwuaji wa jarida
Mnamo terehe 24 Aprili 2010, TUSIMA ilichanja mbuga mpya katika maendeleo ya shirika la Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya kushuwa jarida lake la mwanzo hapo Ngome ya Yesu Mombasa mgeni mheshimiwa akiwa ni Bwana Issa Timami ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya. Jarida hili liliwezeshwa kwa ufadhili wa kampuni ya Fairdeak Holdings. Miongoni mwa waliohudhuriaya ni pamoja na mkurugenzi Mkuu wa MKK Daktari Idle Farah Omar , Profesa Mohamed Abdulaziz, Washauri wa TUSIMA, Bwana Hussein Zakir Mkurugenzi wa fairdeal, Bwana Mahmoud Noor wa SEACOM na wengineo. Mbali na jarida hilo TUIMA iliweza piya kushuwa tovuti yake mpya www.rissea.org ambayo ilitengezwa upya kwa msaada wa SEACOM, kampuni ya Just Imaging na Kenay Data Network.

Kaimu Mkurugenzi wa TUSIMA alitowa nasaha kuwa jarida hili jipya litakuwa silakuelimisha jamii pekee kuhusu ratiba na taratibu za TUSIMA bali litakuwa chomba muhimu kuwaunganisha jamii, wasomi na watafiti mbali mbali kutuma nakala kumbatana na mipango ya TUSIMA
Wageni waalikwa wakilipitia jarida jipya la TUSIMA


SANAA NA UFUNDI WA WASWAHILI

Ufundi wa ushonaji chuoni TUSIMA
Taasisi ya Utafiti wa Waswahili ya Mashariki mwa Africa - TUSIMA ina vyuo mashuhuri  vya  ufundi wa Waswahili - Mombasa na Lamu ambazo huwawezesha vijana kutukuwa masomo ya ufundi yenye kiwango cha shahada. Masomo yenyewe ni kuwafundisha wanafunzi kutema mbao wakifunzwa nakshi za kibajuni, kigujarati, kiomani n.k, pia humuwezesha mwanafunzi kujuwa useremala kamili. Kwa upande wa kike, wanafunzi hufunzwa kushona nguo za kila mapambo, kutia darizi, kutia vito kofia za Kiswahili n.k. Kuna wale wanafunzi wakushinda kutwa na pia kuna wa koto(part-time). Kila mwaka TUSIMA hutowa matangazo kupitia vyombo mbali mbali vya habari kwa kujiandikisha kwa kozi zetu. Na mahitaji nikama ifuatayo:
Barishiti na forona zilizotiwa darizi

  • Awe ni raia wa Kenya na mwenye umri wa kati ya 16 mpaka 25
  • Awe amemaliza kuwango cha elimu ya shule ya msingi ama zaidi
  • Kosi inategemea uwezo wa fahamu ya mtu ni kutoka mwaka moja hadi miwili
Mipango kabambe inaandaliwa kukifanya chuo kuwa na uwezo wakusajili wanafunzi wa shahada ya Diploma kupitia ya ushirika wa vyuo vengine vikuu vya elimu humu nchini. Kosi hizi ziliundwa sikwaajili kuhuhisha turathi za Kiswahili peke bali pia ni kuhifadhi na kulinda mila na desturi za wa Waswahili wasehemu zote za miji ya kale hadi mji mkongwe Zanzibar
Kazi za mbao chuoni TUSIMA

JAMII YA MALINIDI WAPOKEYA TAMASHA LA KWANZA LA KITAMADUNI LA MALINDI KWA SHANGWE

Ngoma za kitamaduni za kimijikenda
Tamasha la kwanza la Malindi lilikuwa la siku tatu kuanziya tarehe Pili hadi Nne ya Aprili 2010. Waandalizi wa tamasha hili walitoka Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya wakiwamo wa TUSIMA na wakiwamo washidau kutoka Malindi na MADCA.

Tamasha hili litakuwa likiandawa kila mwaka kwa shabaha ya kuhuisha turathi za kitamaduni ambazo zinapoteya kwa haraka sana kutokana na athari za kigeni. Pia ni fursa kubwa kuzileta pamoja jamii zote zinazoishi Malindi ilikuonesha turathi tafauti na pia kuendeleza amali zoa zinazohusiana na turathi.

Shamra shamra nyingi zilikuwako wakati wa tamsha hili ikiwamo moenesho ya vakula va asili, ngoma za kienyeji, sanaa za kiasili, michezo kwa vijana na mashindano ya mashua, uvuvi na upakaji wa hina.Pia kuliandaliwa warsha iliyosimamiwa na kuongoza na TUSIMA 

Bali na hayo wanawake hawakuwacha nyuma siku hiyo walionyesha ngoma mbali mbali za wanawake kama lelemama na vugo. Pia walisaidiya kuwavisha kiasili wasichana katika maonesho ya kujitanda leso. 
Goma kutoka Malindi

Tamasha zenyewe zilisambazwa katika maeneo kadha ya Malindi moja wapo ni Jengo lazamani la Ofisa wa Taarafa ambapo maonesho ya sana za kiasili zilitandikwa hapo na pia maenyesho ya leso tofauti tofauti zilizodhaminiwa na mwana biashara maarafu wa leso Bwana Abdalla Leso. Na kiwanja cha mpira kilioka mbele ya makumbusho ya Malindi. Sehemu hii kila aina za ngoma za kienyeji zilioneshwa na kuwatumbuiza wageni.


Mashindano ya uvuvi wakati wa tamasha

MAONESHO YA SOKO TEMBEZI LA 2010

Maonyesho ya Soko Tembezi katika Village Market Nairobi ni hatuwa muhimu katika kuleta biashara ya vitu pamoja na huduma mbali mbali katika makusanyiko mamoja. Soko hili liliazimiya kuwapa fursa muhimu wahudumu wa sekta ya utalii nafasi ya kufanya biashara na ulimwengu wote. TUSIMA ilishiriki miongoni mwa washirika wengine 55 na kila mmoja alionyesha vitu vyake huku akitumainiya wateja kununua bidha hizo.

Maonesho ya vyombo vya Kiswahili katika soko tembezi Village Market Nairobi
Lengo la kushiriki kwa RISSEA ilikuwa ni  kupanua fikra za kibiashara na kugundua masoko mapya. Hivo basi, tulianika vyombo maridadi vya Kiswahili na kazi ashiki za darizi ili kupata wateja na huku tukijifunza kutoka kwa wenzetu.

Kuwahudumiya kikamilifu wateja wetu ndilo lengo na shabaha yetu. Bidhaa zetu zinapatikana katika Makumbusho ya Nairobi na katika afisi zetu za TUSIMA Mombasa na Lamu.