Wednesday, September 15, 2010

MWITO WA IKHTISARI WAKOMA

Jumba la ofisi kuu ya RISSEA
Kadhiya ya mwito wa ikhtisari kwa kongamano la kimataifa la RISSEA litakalofanyika hapo Novemba mwaka huu umekoma. Jumla ya ikhtisari 25 zilipitishwa na Kamati ya Urejelezi na waliyofaulu tayari wameshajulishwa kutayarisha makala zao kamili. Mawanda yaliyogusiwa kuligana na ikhtisari hizo ni pamoja na ilimu insi, isimu, historiya, fasihi, dini na uchumi wa ardhi. Makala kamili yanatarajiwa mnamo tarehe 8 mwezi wa Novemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment