Bwana Harusi akiwa na vazi la joho |
Maonesho haya yaliyoandaliwa na wachapishaji wa jarida la EVE yaliazimiya kuwaleta wapambaji pamoja na washonaji wa nguo na mapambo mengine ya maharusi kuonesha bidha hizo ili wapate kujulikana na kujenga uhusiano na wateja wapya. Maonesho haya yalifanyika kuanziya tarehe 10 hadi 12 Septemba 2010.
TUSIMA ilionesha mavazi ya bwana na bibi harusi wa Kiswahili yakiwamo majoho, magauni, vibeti, mikoba, marinda na bidhaa nyinginezo za maharusi. Wageni wengi walitembeleya maandalizi ya TUSIMA na kupendezewa nayo. Wawakilishi wa TUSIMA walijijulisha kwa wateja wengi wapya ambao walifurahiya bidhaa hizo. Wawakilishi hawa walitiwa moyo sana na maonesho haya hata wakahamasika kufanya yao au kushiriki tena katika maonesho kama haya mwakani.
No comments:
Post a Comment