 |
Wageni mashuhuri waliohudhuri tamasha za ushwuaji wa jarida |
Mnamo terehe 24 Aprili 2010, TUSIMA ilichanja mbuga mpya katika maendeleo ya shirika la Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya kushuwa jarida lake la mwanzo hapo Ngome ya Yesu Mombasa mgeni mheshimiwa akiwa ni Bwana Issa Timami ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya. Jarida hili liliwezeshwa kwa ufadhili wa kampuni ya Fairdeak Holdings. Miongoni mwa waliohudhuriaya ni pamoja na mkurugenzi Mkuu wa MKK Daktari Idle Farah Omar , Profesa Mohamed Abdulaziz, Washauri wa TUSIMA, Bwana Hussein Zakir Mkurugenzi wa fairdeal, Bwana Mahmoud Noor wa SEACOM na wengineo. Mbali na jarida hilo TUIMA iliweza piya kushuwa tovuti yake mpya www.rissea.org ambayo ilitengezwa upya kwa msaada wa SEACOM, kampuni ya Just Imaging na Kenay Data Network.
Kaimu Mkurugenzi wa TUSIMA alitowa nasaha kuwa jarida hili jipya litakuwa silakuelimisha jamii pekee kuhusu ratiba na taratibu za TUSIMA bali litakuwa chomba muhimu kuwaunganisha jamii, wasomi na watafiti mbali mbali kutuma nakala kumbatana na mipango ya TUSIMA
 |
Wageni waalikwa wakilipitia jarida jipya la TUSIMA
|
No comments:
Post a Comment