Ngoma za kitamaduni za kimijikenda |
Tamasha la kwanza la Malindi lilikuwa la siku tatu kuanziya tarehe Pili hadi Nne ya Aprili 2010. Waandalizi wa tamasha hili walitoka Makumbusho ya Kitaifa ya Kenya wakiwamo wa TUSIMA na wakiwamo washidau kutoka Malindi na MADCA.
Tamasha hili litakuwa likiandawa kila mwaka kwa shabaha ya kuhuisha turathi za kitamaduni ambazo zinapoteya kwa haraka sana kutokana na athari za kigeni. Pia ni fursa kubwa kuzileta pamoja jamii zote zinazoishi Malindi ilikuonesha turathi tafauti na pia kuendeleza amali zoa zinazohusiana na turathi.
Shamra shamra nyingi zilikuwako wakati wa tamsha hili ikiwamo moenesho ya vakula va asili, ngoma za kienyeji, sanaa za kiasili, michezo kwa vijana na mashindano ya mashua, uvuvi na upakaji wa hina.Pia kuliandaliwa warsha iliyosimamiwa na kuongoza na TUSIMA
Bali na hayo wanawake hawakuwacha nyuma siku hiyo walionyesha ngoma mbali mbali za wanawake kama lelemama na vugo. Pia walisaidiya kuwavisha kiasili wasichana katika maonesho ya kujitanda leso.
Goma kutoka Malindi |
Tamasha zenyewe zilisambazwa katika maeneo kadha ya Malindi moja wapo ni Jengo lazamani la Ofisa wa Taarafa ambapo maonesho ya sana za kiasili zilitandikwa hapo na pia maenyesho ya leso tofauti tofauti zilizodhaminiwa na mwana biashara maarafu wa leso Bwana Abdalla Leso. Na kiwanja cha mpira kilioka mbele ya makumbusho ya Malindi. Sehemu hii kila aina za ngoma za kienyeji zilioneshwa na kuwatumbuiza wageni.
Mashindano ya uvuvi wakati wa tamasha |
No comments:
Post a Comment